Pages

Slider

Thursday, December 30, 2021

Tisha na Tembocardvisa yafanikisha miamala ya mabilioni

Mwandishi Wetu.
Mwezi mmoja tangu izinduliwe kampeni ya “Tisha na TemboCardVisa” katika mikoa ya kanda ya kaskazini inayolenga kuhamasisha miamala ya kidijitali, mwitikio wa wateja umefanikisha miamala ya mabilioni mpaka sasa.

Kwa kushirikiana na kampuni ya Visa International, Benki ya CRDB ilizindua kampeni hiyo Desemba mosi 2021 ukiwa ni utekelezaji wa mkakati wa kujenga utamaduni wa kufanya miamala ya kidijitali huku wateja wanaoshiriki hilo wakijiweka kwenye nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwamo kwenda kushuhudia kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) litakalofanyika nchini Cameroon mwaka 2022.

Tangu kuzinduliwa kwa kampeni hiyo katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kulikojumuisha matangazo ya barabarani, uwezeshaji wa vituo vya huduma zikiwamo baa, Migahawa, vyuo vikuu, maduka ya rejareja na supermarkets na michezo hasa riadha, pamoja na ziara kwenye vyombo vya habari, Jumla ya miamala 136 yenye thamani ya Sh17 bilioni imefanyika.

Kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata taarifa za kampeni hii, maofisa wa Benki ya CRDB walitembelea vyombo vya habari wakianza na kituo cha Sunrise FM cha jijini Arusha. Maofisa hao walienda katika kituo hicho Desemba 10 mwaka 2021 na kutoa elimu kwa wananchi.
Licha ya kuzungumza na wananchi wa kituo hicho cha redio, huduma ya kulipa kwa kadi ilizinduliwa Pillars ambako maofisa wa benki walizungumza na wateja.
“Licha ya kuzungumza na wateja, tulitoa zawadi kuonyesha shukrani kwao kwa kuendelea kutumia huduma zetu,” anasema Erica Mwaipopo, meneja mwandamizi wa biashara ya kadi Benki ya CRDB. 
Maeneo mengine ambako huduma ilizinduliwa ni katika vituo vya mafuta kikiwamo cha Great North.
 
Wateja wanaoenda katika maeneo mbalimbali kufanya manunuzi ikiwamo TFA Mall nao wanaweza kuitumia huduma yetu kwani inapatikana hapo. Wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (Muco zamani Muccobs) mkoani Kilimanjaro nao wameunganishwa ambapo kunakipengele kinacho jitegemea kwenye promosheni hii mahsusi kwa wanafunzi. Mjini Moshi, huduma hii ya kulipa kwa kutumia kadi ya TemboCardVisa inapatikana katika kituo cha Mafuta cha Oryx, Kilimanjaro Star Supermarket pamoja na baa za Kwetu Pazuri na Redstone.

Desemba 24, Erica Mwaipopo alitoa elimu kwa wananchi wa Kilimanjaro wanaosikiliza Redio ya Kili FM na wateja waliokuwepo Kwetu Pazuri, Hugo’s Garden, Kilimanjaro Star Supermarket, Redstone na Kili Home Recreation Centre walianza kunufaika na huduma hii salama na ya uhakika baada ya kuzinduliwa katika vituo hivyo huku magari ya matangazo yakizunguka mitaani kuwahamasisha na kuwawezesha wananchi kuitumia.
Wiki tatu za kujumuika na wateja, wadau na wananchi wa kanda ya kaskazini zilihitimishwa Desemba 26 ambapo elimu ilitolewa kuhusu promosheni hiyo kwa washiriki wa Siha Marathon zilizodhaminiwa na Benki ya CRDB na kampeni ya Tisha na TembocardVisa ikaongeza uhai na kunogesha mashindano hayo.
Akihimiza umuhimu wa kufanya miamala kidijitali, Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya CRDB, Boma Raballa alisema matumizi ya Huduma za Tehama yanatokana na mabadiliko ya teknolojia yanayoshuhudiwa duniani kote hivyo kurahisisha biashara hata katika kipindi cha changamoto kama janga la Uviko-19.

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo iliyofanyika makao makuu ya CRDB jijini Dar es Salaam, Raballa alisema wateja watakaotumia zaidi kadi zao watajiweka kwenye nafasi ya kujishindia zawadi katika kipindi chote cha kampeni itakayohitimishwa Machi 2022.

“Lengo letu ni kuona Watanzania wanajenga utamaduni wa kutumia kadi zao kufanya malipo ya huduma au bidhaa wanazonunua na kuachana na utaratibu wa kutumia pesa taslimu. Katika kipindi chote cha kampeni tutatoa zawadi kwa zaidi ya washindi 80, kila mwezi tutakuwa na washindi 20,” alisema Raballa.
Kati ya zawadi ambazo wateja wanaendelea kujizolea ni kurudishiwa asilimia tano ya kiasi walichotumia, kulipiwa bili ya ununuzi walioufanya, simu janja, tablet, televisheni, seti ya sofa, home theatre, na safari ya kitalii kwenda Zanzibar au Serengeti. 

Lakini, zawadi kubwa zaidi, ni safari ya kwenda Cameroon kushuhudia michuano ya AFCON. Wateja wanne watakaofanya miamala mingi zaidi kati ya Desemba 2021 na Januari 2022 wataenda Cameroon, wakipenda wanaweza kuambatana na wenza au rafiki zao, aliongeza Raballa.

Kwa wapenzi wa michezo hasa mpira wa miguu, hakuna muujiza wa kuishuhudia michuano hiyo chini ya udhamini wa Benki ya CRDB zaidi ya kushiriki kampeni hiyo kwa kutumia kadi ya TembcardVisa kufanya malipo na kuuendeleza na kujenga utamaduni huo wa kufanya miamala pasipo kutumia fedha taslimu.

Kwa wasio na akaunti ya Benki ya CRDB, wanashauriwa kufungua ili waweze kuunganishwa na TembocardVisa na kuanza kufurahia huduma hii makini huku wakijiwekea nafasi ya kujishindia zawadi zinazoendelea kutolewa na Benki hiyo. “Tumerahisisha ufunguaji wa akaunti, Kama una simu janja, pakua program ya SimBanking na ufuate hatua za kufungua akaunti ukitumia namba ya kitambulisho cha Taifa kisha omba Tembocard. Kwa wasio na simu janja wanaweza kwenda kwa wakala wa CRDB wakiwa na kitambulisho cha Taifa ili waweze kufunguliwa akaunti na kupata TemboCardVisa,” alisema Raballa.

Jinsi ya kushiriki

Ili kuwa miongoni mwa washindi, Erica Mwaipopo anasema mteja anatakiwa kutumia kadi yake ya TemboCardVisa kulipia bidhaa au huduma anazopata dukani, supermarket, mgahawani/hotelini au hata kwenye vituo vya mafuta, baa na anapofanya malipo mtandaoni ikiwamo kulipia tiketi za ndege au kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi.

Kampeni ya “Tisha na TemboCardVisa” inaenda sambamba na uzinduzi wa muonekano mpya wa kadi za CRDB TemboCard zilizoboreshwa zaidi ili kuwapa wateja uzoefu bora zaidi pindi wazitumiapo.

Kuhusu mwonekano huo mpya, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya CRDB, Joseline Kamuhanda anasema zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa inayowawezesha wateja kuzitumia kwa urahisi mahali popote.

CRDB ilikuwa Benki ya kwanza kuanzisha matumizi ya kadi za kutolea fedha nchini ilipozindua TemboCard mwaka 2002. Mpaka sasa imetoa zaidi ya TemboCard milioni tatu huku ikiungana na mifumo ya malipo ya kimataifa ya Visa, MasterCard na Union Pay.  

Licha ya kulipa kirahisi kwenye maelfu ya vituo vilivyopo nchini, mteja wa Benki ya CRDB iliyoanzishwa mwaka 1996 wanaweza kuzitumia kadi zao kwenye mashine zaidi ya 460 za kutolea fedha nchini (ATM) na mashine 15 za kuweka hela.

Benki hiyo yenye matawi 198 nchini kote pamoja na matawi 12 yanayotembea, inawaruhusu wateja wake kulipia bidhaa au huduma kwenye takriban vituo 990 vilivyopo na kupata huduma kutoka kwa zaidi ya 1,769 mawakala. 

Nje ya mipaka, wateja wa Benki ya CRDB wanaweza kuhudumiwa nchini Burundi ambako ina kampuni tanzu huku ikikamilisha utaratibu wa kuanza kutoa huduma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Vilevile, wateja wanaweza kununua bidhaa mtandaoni kutoka mahali popote duniani walikojiridhisha na ubora wa bidhaa husika kasha kulipa kwa kutumia kadi ya Benki ya CRDB.

Friday, November 16, 2012

HUAWEI YAZINDUA MPANGO WA TEKNOHAMA KATIKA SEKTA YA ELIMU NCHINI

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa mpango kabambe wa Teknohama katika Sekta ya Elimu nchini uliofadhiliwa na Kampuni ya HUAWEI kutoka China leo.
Katika Mradi huo wa Teknohama itayowezesha Watanzania mbalimbali kutoka shule za Sekondari na Vyuoni kupata vifaa na mafunzo ya Sayansi na Teknolojia ili kusukuma mbele maendeleo katika nyanja za Uchumi na Kijamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUAWEI kutoka China Bw. Bruce Zhang akizungumza katika hafla hiyo kwamba Mpango huu unaoitwa "Huawei ICT Star" itasaidia katika shule za Primary na Sekondari katika kusukuma mbele maendeleo ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania.
Alisema katika Program hii itasaidia kuboresha miundo mbinu katika Sanyansi na Teknolojia ili kutoa mwamko kwa vijana wa Kitanzania kujifunza masomo ya Sayansi na Teknolojia.
Balozi wa China nchini Tanzania Mh. LU YOUQING akitoa maelezo yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa Teknohama katika shule na vyuo nchini Tanzania.
Balozi alisema mpango huu ni mwendelezo wa uhusiano mwema kati ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa China katika nyanja mbalimbali za biashara uchumi na Kijamii.
Aliongeza kwamba Serikali ya China itaendelea na mikakati yake ya kusaidia nchi ya Tanzania ili kuweza kufikia malengo ya Milenia ya 2015.
Meza Kuu.
Mgeni rasmi Mh. Mbarawa na Balozi wa China wakizindua rasmi mpango wa "HUAWEI ICT STAR" nchini Tanzania.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Mbarawa na Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI Bw. Bruce Zhang wakitiliana saini kitabu cha makubaliano rasmi ya Ushirikiano katika Sekta ya Sayansi na Teknolojia kupitia Elimu.
Profesa Mbarawa akimkabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI.
Pichani Juu na Chini ni wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
Mgeni rasmi Waziri Mbarawa akiondoka ukumbi baada ya uzinduzi.

HUAWEI YAZINDUA MPANGO WA TEKNOHAMA KATIKA SEKTA YA ELIMU NCHINI

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa mpango kabambe wa Teknohama katika Sekta ya Elimu nchini uliofadhiliwa na Kampuni ya HUAWEI kutoka China leo.
Katika Mradi huo wa Teknohama itayowezesha Watanzania mbalimbali kutoka shule za Sekondari na Vyuoni kupata vifaa na mafunzo ya Sayansi na Teknolojia ili kusukuma mbele maendeleo katika nyanja za Uchumi na Kijamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUAWEI kutoka China Bw. Bruce Zhang akizungumza katika hafla hiyo kwamba Mpango huu unaoitwa "Huawei ICT Star" itasaidia katika shule za Primary na Sekondari katika kusukuma mbele maendeleo ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania.
Alisema katika Program hii itasaidia kuboresha miundo mbinu katika Sanyansi na Teknolojia ili kutoa mwamko kwa vijana wa Kitanzania kujifunza masomo ya Sayansi na Teknolojia.
Balozi wa China nchini Tanzania Mh. LU YOUQING akitoa maelezo yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa Teknohama katika shule na vyuo nchini Tanzania.
Balozi alisema mpango huu ni mwendelezo wa uhusiano mwema kati ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa China katika nyanja mbalimbali za biashara uchumi na Kijamii.
Aliongeza kwamba Serikali ya China itaendelea na mikakati yake ya kusaidia nchi ya Tanzania ili kuweza kufikia malengo ya Milenia ya 2015.
Meza Kuu.
Mgeni rasmi Mh. Mbarawa na Balozi wa China wakizindua rasmi mpango wa "HUAWEI ICT STAR" nchini Tanzania.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Mbarawa na Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI Bw. Bruce Zhang wakitiliana saini kitabu cha makubaliano rasmi ya Ushirikiano katika Sekta ya Sayansi na Teknolojia kupitia Elimu.
Profesa Mbarawa akimkabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI.
Pichani Juu na Chini ni wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
Mgeni rasmi Waziri Mbarawa akiondoka ukumbi baada ya uzinduzi.

HUAWEI YAZINDUA MPANGO WA TEKNOHAMA KATIKA SEKTA YA ELIMU NCHINI

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa mpango kabambe wa Teknohama katika Sekta ya Elimu nchini uliofadhiliwa na Kampuni ya HUAWEI kutoka China leo.
Katika Mradi huo wa Teknohama itayowezesha Watanzania mbalimbali kutoka shule za Sekondari na Vyuoni kupata vifaa na mafunzo ya Sayansi na Teknolojia ili kusukuma mbele maendeleo katika nyanja za Uchumi na Kijamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUAWEI kutoka China Bw. Bruce Zhang akizungumza katika hafla hiyo kwamba Mpango huu unaoitwa "Huawei ICT Star" itasaidia katika shule za Primary na Sekondari katika kusukuma mbele maendeleo ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania.
Alisema katika Program hii itasaidia kuboresha miundo mbinu katika Sanyansi na Teknolojia ili kutoa mwamko kwa vijana wa Kitanzania kujifunza masomo ya Sayansi na Teknolojia.
Balozi wa China nchini Tanzania Mh. LU YOUQING akitoa maelezo yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa Teknohama katika shule na vyuo nchini Tanzania.
Balozi alisema mpango huu ni mwendelezo wa uhusiano mwema kati ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa China katika nyanja mbalimbali za biashara uchumi na Kijamii.
Aliongeza kwamba Serikali ya China itaendelea na mikakati yake ya kusaidia nchi ya Tanzania ili kuweza kufikia malengo ya Milenia ya 2015.
Meza Kuu.
Mgeni rasmi Mh. Mbarawa na Balozi wa China wakizindua rasmi mpango wa "HUAWEI ICT STAR" nchini Tanzania.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Mbarawa na Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI Bw. Bruce Zhang wakitiliana saini kitabu cha makubaliano rasmi ya Ushirikiano katika Sekta ya Sayansi na Teknolojia kupitia Elimu.
Profesa Mbarawa akimkabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI.
Pichani Juu na Chini ni wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
Mgeni rasmi Waziri Mbarawa akiondoka ukumbi baada ya uzinduzi.

Tuesday, March 13, 2012

Kamera Ya Mtaa Kwa Mtaa na Matukio Mbali Mbali ya jijini Dar leo

Waendesha Boda Boda wakiwa kwenye msafara wa kwenda mazikoni kumsindikiza mwenzao aliefariki Dunia kwenye nyumba yake ya milele.
 Kama kawaida,Jiji letu ikinyesha mvua hata kama ni lita mbili,maji ni kila kona na hayaondoki kwa haraka.
 Mbuzi wa Mzee nanihii wakiliendeleza libeneke la Mtaa wa Mtaa kama walivyonaswa leo na Kamera yetu.
 Mdau akitolea macho taka taka pembezoni mwa mtaro wa maji machafu maeneo ya Mikocheni A usoni mwa Mayfar Plaza.
 Nani kasema Bajaj inakwenda bila kidebe?
 Maghorofa yetu ya Kisasa yalivyojengwa.
 Pamoja na kwamba kuna kihifadhia taka lakini bado nyingine nyingi zipo chini.
 Wazee wa Long Parking jijini Dar wakimchimba mkwala dereva alieegesha sehemu isiyo rasmi (japo hakuna ishara yeyote inayoonyesha kama hapo sio sehemu rasmi kwa kuegesha gari).
 kama kawa kama dawa.
 Fundi akisubiria wateja.
Bustani ya Posta ya Zamani.
Blog Designed by The Single Momoirs